BETWAY NDIYO MDHAMINI MKUU WA SIMBA SC KWA MIAKA MITATU

 


Klabu ya mpira wa miguu nchini Tanzania, Simba Sports Club imepata mdhamini mkuu mpya, ambapo mdhamini hiyo ni kampuni ya kubashiri ifahamikayo kwa jina la BetWay

Aidha kampuni hiyo ya kubashiri imeingia mkataba wa kuwa mdhamini mkuu wa club hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu yaani kuanzia msimu wa 2025/26 mpaka msimu wa 2027/28

Hii ni baada ya kampuni ya M-bet ambayo ilikuwa mdhamini wa Simba kuanzia 2022 kusitisha mkataba na club hiyo namba tano kwa ubora barani Afrika.

Hata hivyo hapo awali, kampuni ya M bet iliingia mkataba wa miaka mitano kuidhamini timu ya simba kwa kuanzia 2022 mpaka 2026 lakini wameshindwana na kuamua kujiweka pembeni.

 

MDHAMINI MPYA

Betway wameingia mkataba wa miaka mitatu na club ya simba na sasa rasmi, simba atakuwa akivalia jezi zenye nembo ya Betway kifuani kuanzia msimu huu 2025/26 mpaka pale kampuni hiyo itakapoachia ngazi ya udhamini ukuu.

 

Vile vile Kampuni imeweka kiasi cha sh Bilioni 20 za kitanzania kwa miaka yote mitatu lakini zikilipwa kwa awamu tatu kwa kila msimu

Pia kampuni na club zimekubaliana kwamba kutakuwa na bonasi mbali mbali zitakazotolewa na mdhamini huyo pindi timu itakapofanya vyema kwenye mashindano, bonas hiyo itategemea na mafanikio ya club.

 

Licha ya kuwa mdhamini mkuu, lakini Betway hatoizuia club ya simba kuwa na wadhamini wengine, ikiwa ni pamoja na matangazo ya biashara za Mo Dewji ambazo zinamilikiwa na muwekezaji Mohamed Dewji mwenye hisa asilimia 49 ndani ya club hiyo.



 

 

 

Hakuna maoni

Picha za mandhari zimetolewa na imagedepotpro. Inaendeshwa na Blogger.